Mchekeshaji Mahiri kutoka nchini Uganda,Anne Kansiime (wa pili kulia) akifafanua jambo mbele ya Wanahabari kuhusiana na burudani kubwa ya uchekeshaji atakayoionyesha kwa mashabiki wake hapo kesho Agosti 2,2014  katika ukumbi wa Golden Tulip,jijini Dar,Kulia kwake ni mchekeshaji mwingine kutoka nchini Kenya,Fred Omondi.
 Mmoja wa wachekeshaji mahiri kutoka nchini Tanzania,atambulikae kwa jina la kisanii Mc Pili Pili akielezea jambo kwenye mkutano wa Wanahabari uliofanyika mapema leo jijini Dar,wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Radio 5, Robert Francis,ambao ndio waandaaji wa Onesho hilo la vichekesho.
 Baadhi ya Wanahabari walioshiriki mkutano huo wa wasanii wa vichekesho uliofanyika mapema leo jijini Dar

========  ======  ====== 

Mchekeshaji Anne Kansiime anatarajiwa kutoa burudani kubwa siku ya Jumamosi kwa mashabiki wake katika ukumbi wa Golden Tulip.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Sports Lounge, mkali huyo wa kuchekesha na sanaa za majukwaani amesema mashabiki wake watarajie mambo makubwa hapo Jumamosi.

‘Hii ni mara yangu ya kwanza kuja Tanzania, hivyo mashabiki wangu watarajie burudani ambayo itaacha mbavu zao hoi, lakini pia watapata nafasi ya kujifunza vitu vingi kupitia vichekesho vyangu’ alisema Anne.

Kwa upande wake, mchekeshaji mwingine kutoka Kenya atayetoa burudani, Fred Omondi, amesema watanzania watarajie burudani kali kama lilivyo jina la burudani yenyewe, Cheka Kwa Nguvu.

‘Usiku wa Jumamosi utawakutanisha moja ya wachekeshaji mahiri barani Afrika, hivyo watanzania waje kwa wingi kushuhudia burudani hii’ alisema Fred.

Naye mchekeshaji Pilipili kutoka Tanzania amesema usiku wa leo utakuwa usiku wa kukumbukwa hasa kwa vichekesho alivyowaandalia mashabiki wake.Usiku wa Cheka Kwa Nguvu unaandaliwa na kituo cha Radio 5 na pia utaambatana na burudani ya muziki kutoka ODAMA Band.

Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Radio 5, Robert Francis amewataka wapenzi wa burudani ya vichekesho kuhudhuria kwa wingi ili wafurahie burudani waliyowaandalia.  ‘Usiku huo utakuwa ni maalumu kwa watanzania kufurahia Utanzania wao, kwani kucheka ni sehemu muhimu kwa maisha ya mwanadamu’ alisema Robert.

Kansiime amejipatia umaarufu kupitia mitandao ya kijamiii ambako alianza kwa kuweka vipande vya video akiigiza kama mwanamke wa kiafrika anayekutana na changamoto mbalimbali za maisha.

Mchekeshaji huyo wa kike, ambaye pia huendesha kipindi cha “Don’t Mess With Kansiime” kwenye kituo cha Citizen TV, anatajwa kuwa mwanamke mwenye kipaji cha pekee nchini Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Please edit...kansime anatokea Uganda sio Kenya

    ReplyDelete
  2. Kansiime anatokea Uganda na sio Kenya. Tafadhali rekebisheni

    ReplyDelete
  3. Taarifa gongana nini,huyo dada ni mganda au mkenya mbona mnatuchanganya waleta taarifa

    ReplyDelete
  4. I wish I could be there. Kansiime madness, no one to compare with her so far. She is a star

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...