Na Veronica Simba
Waziri wa Nishati na Migodi wa Burundi, Mhe. Côme Manirakiza na
Ujumbe wake wako katika ziara ya siku tano (24 – 28 Agosti, 2014)
hapa nchini kwa lengo la kujifunza namna Sekta za Nishati na Madini
zinavyofanya kazi.
Katika ziara yake, Waziri Manirakiza ametembelea Makao Makuu ya
Wizara ya Nishati na Madini – Dar es Salaam na kukutana na Wataalamu
mbalimbali wa Wizara na Taasisi zilizo chini yake wakiongozwa na Kaimu
Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje.
Wakiwa Wizarani, Waziri na Ujumbe wake walipata fursa ya kusikiliza
mada zinazohusu Sekta za Nishati na Madini zilizowasilishwa na
Wataalamu wa Wizara.
Ujumbe huo pia umepata nafasi kutembelea Taasisi na Mashirika
mbalimbali yaliyo chini ya Wizara na yale yenye uhusiano na Wizara
ikiwemo Mpango wa Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia ya Uziduaji
Tanzania (Tanzania Extractive Industry Transparency Initiative – TEITI),
Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasimali Madini (SMMRP) na Wakala
wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA).
Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje akiwasilisha mada
kuhusu Sekta ya Madini – Tanzania kwa Waziri wa Nishati na Migodi
wa Burundi, Mhe. Côme Manirakiza (wa kwanza kulia) na Ujumbe wake
(Kulia kwake) waliofika Makao Makuu ya Wizara – Dar es Salaam, Agosti
26, 2014 kujifunza namna Sekta za Nishati na Madini zinavyofanya kazi.
Upande wa kushoto ni Wataalamu mbalimbali wa Wizara na Taasisi zilizo
chini yake.
Mtaalamu kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC),
Wellington Hudson akitoa mada kuhusu Rasilimali za Gesi na Mafuta
kwa Waziri wa Nishati na Migodi wa Burundi, Mhe. Côme Manirakiza
(Wa kwanza Kulia) na Ujumbe wake. Ujumbe huo ulifika Makao Makuu
ya Wizara – Dar es Salaam, Agosti 26, 2014 kujifunza kuhusu Sekta za
Nishati na Madini zinavyofanya kazi. Wengine pichani ni Wataalamu wa
Wizara na Taasisi zilizo chini yake wakiongozwa na Kaimu Kamishna wa
Madini, Mhandisi Ally Samaje (wa kwanza kushoto).
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Profesa Abdulkarim
Mruma (aliyeinua mikono), akitoa ufafanuzi kuhusu GST kwa Waziri wa
Nishati na Migodi wa Burundi, Mhe. Côme Manirakiza (Wa kwanza Kulia)
na Ujumbe wake waliofika Makao Makuu ya Wizara - Dar es Salaam,
Agosti 26 kujifunza namna Sekta za Nishati na Madini zinavyofanya kazi.
Mtendaji Mkuu wa Jiolojia na Migodi (Geology and Mines) wa Burundi,
Emmanuela Ngenzebihoro (mwenye kilemba) akiuliza swali kwa
Wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini – Tanzania (Walioketi
Kushoto), wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati na Migodi wa Burundi,
Mhe. Côme Manirakiza (Wa kwanza Kulia) na Ujumbe wake Makao
Makuu ya Wizara - Dar es Salaam, Agosti 26, 2014. Waziri Manirakiza na
Ujumbe wake walifika wizarani kujifunza namna Sekta za Nishati na Madini
zinavyofanya kazi.
Waziri wa Nishati na Migodi wa Burundi Mhe. Côme Manirakiza (aliyeinua
mkono), akiomba kupewa ufafanuzi kuhusu sekta ya madini hapa nchini,
baada ya uwasilishwaji mada zilizohusu sekta za nishati na madini za
Tanzania. Waziri Manirakiza na Ujumbe wake walitembelea Makao Makuu
ya Wizara ya Nishati na Madini - Dar es Salaam, Agosti 26, 2014 kwa
lengo la kujifunza namna sekta husika zinavyofanya kazi. Wengine pichani
ni Wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini - Tanzania (kushoto) na
Ujumbe ulioongozana na Waziri (Kulia).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...