Marehemu Mzee Joseph Mturi Mahemba
(1955-2012)
Mpendwa Baba yetu, Joseph Mturi Mahemba
Hatimaye siku, Miezi imepita hadi hii leo ambapo imetimia Miaka miwili (2) tangu ulipotutoka
ghafla usiku ule wa siku ya jumatano ya tarehe moja ya Mwezi Agosti, 2012 na kutuachia
huzuni kubwa.
Japokuwa haupo nasi hapa duniani lakini tupo nawe kiroho kwa kuendeleza mema yote
uliyotufundisha na kutuasa.
Tunakukumbuka kwa Upole, Upendo, Busara na Ukarimu uliokuwa nao kwa familia na Marafiki.
Mwongozo na matendo yako yataendelea kuwa dira kwetu
Daima unakumbukwa sana na Mkeo Rose Joseph, dada zako Theresia, Karaghita, Wankuru
na Mnaga, wanao wapendwa Michael, Mkami, Niwa, Sagana, Mary, Geofrey, Nyakaho,
Lecardia na Pricilla, na wajukuu zako wote.
Ibada Maalum ya Maombi itafanyika tarehe 03/08/2014 Saa 2.00 asubuhi kwenye kanisa
katoliki la Mt Maurus Kurasini, Dar es Salaam.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa jina lake libalikiwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...