Kikwete na mtangazaji wa Cloud FM Mbwiga MbwigukeRais Dkt. Jakaya Kikwete akipozi katika picha na Mbwiga wa Mbwiguke wa Clouds fm (kulia)

Na Maregesi Paul

SIKU moja nilikuwa katika mkutano wa Jukwaa la Wahariri ambao mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginard Mengi.Katika mazungumzo yake, Mengi aligusia historia ya maisha yake ambapo alisema alikulia katika familia masikini.Kwa mujibu wa Mengi, nyumba aliyokulia ilikuwa na panya wengi pamoja na mende na kwamba kila walipokuwa wakilala usiku, wapita njia walikuwa wakiwaona kwa sababu nyumba ilikuwa imejaa matobo.

Pamoja na mazingira hayo, Mengi kwa sasa ni kati ya matajiri wakubwa wanaoheshimika ndani na nje ya nchi na suala la umasikini aliokulia, limebaki kuwa historia.Hivyo hivyo, hata mimi niliyeandika makala haya, niliwahi kuvua dagaa na sangara kwa kutumia nyavu haramu ziitwazo makokoro. Lakini sasa mimi ni mhariri wa gazeti hili na suala la uvuvi, limebaki katika historia.

Wakati hayo yakitokea, katika Radio Clouds kuna watangazaji wengi wanaovuta masikio na hisia za wasikilizaji kutokana na lugha na vichekesho wanavyovitumia pindi wanapokuwa studio.
Miongoni mwao ni Said Seleman maarufu kwa jina la Mbwiga wa Mbwiguke.

Kama ilivyo kawaida kwa watu kuwa na historia tofauti tofauti kama nilivyoeleza hapo awali, wakati wa mahojiano maalum na MTANZANIA Jumatatu, Mbwiga anaeleza kwa kirefu ni wapi alikotokea hadi akawa mmoja wa watangazaji maarufu katika radio hiyo maarufu nchini.

“Kwanza nianze na maana ya jina Mbwiga. Mbwiga ni neno la kizaramo ambalo maana yake ni rafiki. Kwa hiyo mimi ni rafiki wa kila mmoja kwa sababu huwa napenda sana kuwachekesha watu.
“Lakini pia, maisha ni mzunguko na kamwe hakuna binadamu anayezaliwa na kujua maisha yake yatakuwaje kwa siku zijazo.

“Kwa maana hiyo, hiki nitakachokieleza ndivyo kilivyo kwa sababu hapa nilipo sikutarajia kama itatokea siku nikawa mmoja wa watu wanaoungwa mkono na mamilioni ya Watanzania.“Kwanza kabisa niseme tu kwamba, mtu aliyenifikisha hapa ni mtangazaji mwenzangu aitwaye Shafii Dauda. Huyu ndiye aliyenileta Clouds baada ya kuniona naweza kuwa na mchango fulani fulani katika redio yetu hii.
“Sikumbuki ni mwaka gani, lakini nakumbuka ni kama miaka mitatu iliyopita, siku moja usiku nilikuwa pale Muhimbili Shule ya Msingi kwenye mazoezi ya mpira unaowahusisha wachezaji wakongwe kama akina Akida Makunda, Mohamed Binda, Idd Moshi, Ally Mayai, Crement Kahabuka, Dua Said na wengineo wengi .

“Siku hiyo nilikuwa sichezi bali nilikuwa shabiki tu nikiwashangilia wenzagu, kwa hiyo, mazoezi yalipomalizika, Shafii Dauda alikuja mahali nilipokuwa na akina Ally Mayai na alitukuta tunacheka,” anasema Mbwiga na kuongeza.“Alipoona tunacheka, akauliza tunacheka nini, Ally Mayai akamwambia huyu jamaa anatuchekesha, hebu mchukue umtumie kwenye kipindi chako kile cha michezo cha saa tatu usiku atakusaidia sana,” anasema Mbwiga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...