Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akiweka jiwe la Msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani –Mziha sehemu ya Magole-Turiani (48.6km) inayojengwa kwa kiwango cha lami.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, mbunge wa Mvomero Amos Makalla, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale akitoa maelezo ya kina kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wa kwanza kulia akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kabla ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km) kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya wakifurahia jamabo na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mheshimiwa Antony Mbasa kabla ya uzinduzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwa pamoja na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kushoto wakifurahia kikundi cha ngoma za asili mara baada ya Mheshimiwa Rais kuwasili Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya kuzindua ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe wa kwanza (kushoto) akizungumza kabla ya uzinduzi rasmi wa barabara ya Magole Turiani. Wa kwanza kulia kwake ni Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi Mhandisi Ndyamukama pamoja na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi na Umeme Dkt. Wiliam Nshama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...