Allan Lucky
Aliyekuwa mtangazaji wa kipindi maarufu cha Televisheni kinachohusiana na maisha ya wanafunzi wawapo shuleni, Allan Lucky a.k.a Rais wa Wanafunzi ambaye kwa sasa anafanya shughuli zake nchini Kenya, ameibuka na kipaji kingine, U-DJ.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Allan Lucky amewaambia mashabiki wake kuwa kila Ijumaa ya kwanza ya mwezi, atakuwa anatoa kupitia Hulkshare mixing mpya kali ambayo mtu yeyote anaweza kui-download na kuisikiliza mahali popote, iwe ni kwenye gari, nyumbani, house party na kadhalika. Unaweza kupitia ukurasa wake wa Hulkshare kupata mixing zote kali kutoka kwake http://www.hulkshare.com/AllanLucky
Mwezi huu ametoa mixing ya nyimbo za zamani za miondoko ya RnB ambazo zilipendwa sana miaka ya 90 na mwanzoni 2000. Unaweza pia kuipata kwa kuingia kwenye link hii: http://www.hulkshare.com/allanlucky/hotshit-mixx-11
Kwa taarifa zaidi,unaweza kutembelea kurasa 
zake za Facebook, Twitter na Instagram.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...