Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, (Kulia), akiteta jambo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Afande Leonard Paul, wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Mfuko huo kwa baadhi ya wachezaji wa timu ya polisi mkoani Morogoro na wajumbe wa  idara ya utumishi wa walimu wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo mkoani Morogoro, Alhamisi Oktoba 23, 2014.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu ya Polisi Morogoro, Jumatano Oktoba 22, 2014, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mfuko huo kwa wachezaji hao na wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, wanaohudhuria semina ya siku moja iliyuoandaliwa na Mfuko huo Mkoani Morogoro
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akizungumza na wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Mfuko huo mjini Morogoro Oktoba 22, 2014. Wajumbe hao wanatarajiwa kubhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo ili kuwaelimisha walimu faida wanazoweza kupata endapo watajiunga na Mfuko huo.

 Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mwanjaa Seme, akiwasalimia walimu ambao ni wajumbe kutoka idara ya utumishi wa walimu wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa wajumbe hao wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na PSPF, ili kuelezea shughuli mbaklimbali na faida unazoweza kupata unapojiunga na Mfuko huo. Semina hiyo ilifanyika mkoani Morogoro
Msanii Mrisho Mpoto, ambaye pia ni balozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akiimba sambamba na baadhi ya walimu na maafisa wa Mfuko huo, wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na PSPF, kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo mkoani Morogoro. Picha na Masogange 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sio kawaida kumwona mjomba kavaa viatu.Kulikoni?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...