Katibu
Mkuu wa Wizara ya mambo ya ndani ya nchi Mbaraka Abdualwakili, akizindua
chapisho la tathmini ya Polisi Jamii nchini, hafla hiyo ilifanyika jana Makao
Makuu ya Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha
Alexander Mpeka – Jeshi la Polisi
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi Bw.
Mbaraka Abdualwakil, Mwakilirishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mawasiliano Sayansi na Teknolojia ambaye
ni Mkurugenzi wa utawala na rasilimali watu, Bi Selina Lyimo wakiwa Naibu
Inspekta Jenerali wa Polisi Abdulrahaman Kaniki pamoja timu iliyoshiriki katika utafiti wa tathmini
ya Polisi jamii. Picha na Alexander Mpeka – Jeshi la Polisi.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi Bw.
Mbaraka Abdualwakil, Mwakilirishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mawasiliano Sayansi na Teknolojia ambaye
ni Mkurugenzi wa utawala na rasilimali watu, Bi Selina Lyimo wakiwa Naibu
Inspekta Jenerali wa Polisi Abdulrahaman Kaniki pamoja makamishina wa Jeshi la Polisi wakati wa
hafla ya makabidhiano ya chapisho la utafiti wa tathmini ya Polisi jamii .
Picha na Alexander Mpeka – Jeshi la Polisi.
======= ======= =======
Na. Tamimu Adam - Jeshi la Polisi.
Jeshi
la Polisi nchini limetakiwa kutumia
matokeo ya utafiti wa tathmini ya Polisi
Jamii uliofadhiliwa na Wizara ya
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kupitia Tume ya taifa ya Sayansi na
teknolojia( COSTECH) katika kuboresha mkakati wa Polisi jamii ili kuimarisha ulinzi
na usalama wa raia na mali zao kwani matokeo hayo yana manufaa makubwa katika
kubaini, kuzuia, na kutanzua uhalifu na kero mbalimbali katika jamii.
Hayo
yalisemwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bi. Selina Lymo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na
teknolojia wakati wa hafla ya kukabidhi chapisho la utafiti
wa matokeo ya tathmini ya Polisi jamii
nchini kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Bw. Mbaraka
Abdulwakili .
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi Bw. Mbaraka Abdulwakili alisema atahakikisha utafiti huo
unafanyiwa kazi ipasavyo na amewataka watendaji wa Jeshi la Polisi kutumia
utafiti huo katika kuimarisha usalama wa raia na mali zao kwa kuwa askari
waliopo hawatoshi na Polisi jamii imeonyesha
mafanikio makubwa katika kuzuia vitendo vya uhalifu na wahalifu.
Naye,
Mtaalum Mwelekezi wa Utafiti wa Tathmini ya Polisi Jamii ambaye pia ndiye
Mtafiti Mkuu Dkt Haji Semboja alisema kuwa utafiti huo
ulifanyika katika kanda saba ambapo matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa
uhusiano wa kiutendaji baina ya wananchi na Jeshi la Polisi umeboreshwa kwa
kiwango kikubwa kupitia dhana ya Polisi jamii.
Alisema
kuwa jambo hilo linasaidia katika kutengeneza mazingira ya amani na hivyo
shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii
zinaweza kuendelea kufanyika bila hofu na kwa uhakika wa ulinzi na usalama.
Aliongeza
kuwa, utafiti huo umeonyesha kwamba, watu wengi wanaamini kuwa, matokeo ya
kuanzishwa kwa Polisi jamii katika maeneo yao
kuna mafanikio makubwa katika kuhimiza na kutia moyo uvumbuzi wa njia
mpya za kukabiliana na vitendo vya uhalifu ambapo wananchi wamekuwa wakihimizwa
utoaji wa taarifa za uhalifu kupitia njia mbalimbali ikiwemo njia ya ujumbe
mfupi.
Naye, Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Abdulrahman Kaniki aliipongeza timu
nzima iliyofanya utafiti huo na kusema kuwa Jeshi la Polisi kama watekelezaji
wakuu wa Programu ya maboresho yaliyojikita
katika mihimili mikuu mitatu ambayo ni Weledi, Usasa na Polisi jamii, wanatambua na kuthamini kazi nzuri
iliyofanywa na watafiti hao na amewaomba kuangalia namna wanavyoweza kufanya
utafiti katika mihimili mingine miwili
iliyobaki ambayo ni Usasa na Weledi ili Jeshi
Polisi liweze kuwa na tathimini
halisi ya Maboresho yake.
Kwa
upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia
(COSTECH) Dr. Flora Tibazarwa alisema kuwa madhumuni ya mpango wa utafiti huo
yalikuwa ni kuimarisha uhusiano baina ya
Jeshi la Polisi na wananchi katika kuzuia na kutatua matatizo ya jamii,
msisitizo ukiwa kuzuia uhalifu kabla haujatokea.
Aliongeza
kuwa matokeo ya utafiti huo yatawasaidia watunga sera na watoa maamuzi kutoa maamuzi
na kutunga sera mbalimbali za usalama wa raia na mali zao kwa faida ya taifa
letu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...