Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia  wakazi wa KIMARA na TABATA; Miji ya Kibaha na Mlandizi mkoani Pwani  kuwa, tangu Jumapili ya Tarehe 01/03/2015 Mtambo wa kuzalisha Maji wa Ruvu Juu  umepata hitilafu baada ya bomba la Majighafi (Raw-Water) kuachia kwenye moja ya chemba ya kuchukulia Maji eneo la Mtamboni.
  
Hali hii imelazimu kuzima Mtambo wa Ruvu Juu. 

Mafundi wa DAWASCO wanaendelea na matengenezo ili kuhakikisha  Huduma ya  Maji inarejea katika hali ya kawaida ifikapo  siku ya Ijumaa 06/03/2015.

Wakazi wa maeneo yafuatayo wameathirika na hitilafu hii; MLANDIZI, KIBAHA, KIBAMBA, MBEZI, KIMARA, UBUNGO, CHUOKIKUU, KIBANGU, RIVERSIDE, BARABARA YA MANDELA, TABATA, NA SEGEREA.

KWA TAARIFA ZAIDI PIGA SIMU KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA NAMBA 022 5500 240-4 au 0658-198889
DAWASCO INAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU AMBAO NI WA DHARULA.

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU
“DAWASCO TUTAKUFIKIA”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Lini mitambo hiyo itapatiwa ufumbuzi? BRN, imefanikiwa? ni kazi kweli kumaliza suala hili la Dawasco

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...