Mkurugenzi wa Bayport Financial Services, John Mbaga, pichani, akizungumza jambo katika uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo ya viwanja katika mradi wa Vikuruti, Kibaha, mkoani Pwani. Uzinduzi huo ulifanyika Ijumaa ya Mei 22, katika Hoteli ya Serena na kuhudhuriwa na watu mbalimbali, wakiwamo viongozi wa serikali. Picha zote na Mpiga Picha Wetu.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaama
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, inayojihusisha na mikopo, imeanzisha huduma mpya ya kukopesha viwanja watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni za kawaida na wajasiriamali wa aina zote.
Kuanzishwa kwa huduma hiyo mpya kumetokana na taasisi hiyo kupania kuboresha maisha ya Watanzania, likiwamo kundi la wajasiriamali ambalo limeendelea kusahauliwa na kampuni nyingi kupewa mikopo.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, akizungumza katika uzinduzi huo, jijini Dar es Salaam.
Ngula, you need to practice reading in Kiswahili more
ReplyDelete