Na Avila kakingo,Globu ya Jamii.
 CHAMA cha wafugaji Tanzania (CCWT),kimewataka wafugaji wote nchini kufanya shughuli zao kwa kufuata sheria, pia hawataki kuona wafugaji wakifanya uonevu wa aina yoyote kwa watu wengine.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT),Magembe Makoye wakati akizungumza na wandishi wa habari katika ukumbi wa Habari MAELEZO leo jijini Da es Salaam.
Makoye Amesema kuwa wafugaji watambue kuwa kunakutegemeana na watu wengine katika kuendesha shughuli zao  bila kuathiri  watu wengine katika jamii.
Pia Makoye amesisitiza kuwa  chama cha wafugaji Tanzania hakitavumilia kuona wafugaji wanakuwa chanzo cha migogoro katika jamii,aidha chama hicho kimetoa wito kwa wafugaji wote Tanzania  kujihadhali  na  watu wanaopita kwao na  kujitambulisha kuwa wao ni viongozi wa chama cha wafugaji Tanzania.
Chama hicho  kimeitaka Serikali itenge  ardhi kwa ajili ya  wafugaji ili kuepuka mwingiliano uliopo sasa wa watu kutokujua mipaka yao na hatimaye kusababisha mapigano na uhasama  miongoni mwa makundi hayo,
suluhu ya migogoro mbalimbali iliyopo kati ya wafugaji na watumiaji wa ardhi katika jamii.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania,Magembe Makoye akizungumza na wandishi wa habari  kushusiana na wafugaji kufanya shughuli zao kwa kufuata sheria za nchi katika ukumbi wa Habari MAELEZO leo jijini Dar es Salaam kulia ni Mkurugezi Msaidizi wa Idara ya HABARI MAELEZO Tiganya Vincent .
Baadhi ya waandishi wa habari (PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...