Wapendwa Watanzania na marafiki popote pale duniani,

Kwa niaba ya uongozi wa Tanzania Global Prayer Movement (TGPM) natoa shukrani za dhati kwa wale wote waliojiunga nasi kwenye maombi ya Jumapili hii na siku zote kuanzia Jumapili July 26 tukiombea utakaso wa kiti cha Raisi, Ikulu, viti vya wabunge na madiwani pamoja na amani wakati vyama vinajipanga sawa sawa na uchaguzi.

Yafuatayo ndiyo tunayoendelea kuombea mpaka siku ya Jumapili Agosti 9 ambapo itakuwa hitimisho la wiki tatu kuombea haya maswala. Endelea kuinua jina la Bwana.

1)   Omba Mungu akupe mzigo wa kuombea nchi yako ya Tanzania.
2)   Ombea amani nchini wakati vyama vinakamilisha uchaguzi wa wagombea wao wa nafasi ya Raisi.
3)   Ombea utakaso wa Kiti cha Uraisi wa Tanzania.
4)   Ombea utakaso wa Ikulu ikiwa ni mahali anapofanyia kazi Raisi wa Tanzania, pamoja na ikulu ndogo mikoani.
5)   Ombea utakaso wa viti vya wabunge na madiwani nchi nzima.
6)   Ombea mgombea Uraisi wa UKAWA kama jina litakuwa limetoka. Kama bado, tutaendelea kuombea amani huku mchakachuo ukiendelea.


Please join us via a prayer conference call this Sunday. To join the conference call every Sunday, please dial (218) 895 9661 and passcode is 222555.  The prayer starts at 9pm Eastern, 8pm central, 7pm Mountain or 6pm Pacific time.

For more information about Tanzania Global Prayer Movement (TGPM), please visit our website at:

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...