FAMILIA ya marehemu mzee Japhet Mbaga, wa Dar es Salaam kwa masikitiko makubwa inatangaza vifo vya kaka zao wapendwa, MICHAEL NA JOHN JAPHET MBAGA, vilivyotokea hapa Dar es slaam siku ya Jumapili na Jumatatu zilizopita.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam, siku ya Alhamisi tarehe 3 Septemba, 2015 saa 10.00 jioni.
Ratiba ya kutoa heshima za mwisho itafanyika siku hiyo hiyo, saa 7.00 mchana nyumbani kwa Mary Rusimbi (Mkurugenzi Mkuu, WOMEN FUND TANZANIA) eneo la Tabata - shule, nyumba za TAZARA.
Baadaye saa 9.00 Ibada ya kuwaaga wapendwa wetu itafanyika Kanisa la KKKT Kijitonyama.
Marehemu MICHAEL NA JOHN JAPHET MBAGA ni kaka wa MARY RUSIMBI, HILLARY MBAGA, ROSE MSHANA (ROZELLA) NA STELLA MBAGA.
"Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina lake na lihimidiwe."
AMINA
AMINA
Poleni sana wafiwa
ReplyDeletePoleni sana wafiwa
ReplyDeleteMUNGU awainue familia na kuwapa subira
ReplyDelete