Sheria za kimataifa hususani kipengele cha 16 cha mkataba wa kimataifa wa kulindwa kwa haki za Mtoto duniani zinaonekana kuvunjwa nchini Israel ambako nchi hiyo inawashikilia mateka Watoto wa Kipalestina wanaokadiriwa kufikia 438 katika magereza yao.

Habari kutoka katika kituo cha utafiti wa mateka wa Kipalestina kinadai kuwahivi karibuni mtoto wa kipalestina Shadi Faraj mwenye umri wa miaka 12 alifikishwa kwenye mahakama moja nchini Israel kwa mara ya tatu na kesi yake kuahirishwa bila kujulikana hasa kosa la mtoto huyo ni lipi.

Kwa mujibu wa mkuu wa kitengo cha habari wa kituo hicho Riyadh Ashqar,amesema katika ripoti yake aliyoituma kwenda kwa manasaba wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupambana na mateso (QUDS) kwamba utwala wa kizayuni wa Israel unatumia mbinu 80 za mateso ya kimwili na kiroho dhidi ya mateka wa Kipalestina.

Ripoti ya hivi karibuni ya mfuko wa Watoto wa U moja wa Mataifa (UNICEF) inaonesha kuwa utawala wa kizayuni wa Israel ndiyo utawala pekee duniani unaowapandisha kizimbani kwa makusudi na kwa lengo maalumu, watoto wadogo tena kwenye mahakama za kijeshi.

Siku hii ya kimataifa ya QUDS huadhimishwa kila mwaka siku ya Ijumaa ya mwisho ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, hii ina maana kesho ndiyo siku yenyewe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...