Baadhi ya wanafunzi tuliosoma Shule ya Sekondari Bwawani tukiwa katika picha ya pamoja wakati wa kuelekea kuitembelea shule yetu hiyo..

Na Josephat Lukaza - Bwawani
Hatimaye waliowahi kusoma na kuhitimu katika Shule ya Sekondari ya Bwawani iliyopo Mkoa wa Pwani wamefanikisha adhma yao ya kuitembelea iliyokuwa shule yao kwaajili ya Kuwatia moyo na amasa vijana wanaoendelea na masomo katika shule hiyo huku wengi wao wakiwa ni vijana wa kidato cha Kwanza hadi cha Nne.

Waliowahi kuwa wanafunzi hao waliwasili majira ya saa sita mchana na kupokelewa na waliokuwa walimu wao kipindi hiko wakiwa wanasoma shule hapo na kupata nafasi ya kuonyeshwa sehemu mbalimbali za shule hiyo huku waliokuwa wanafunzi katika shule wakipata nafasi pia ya Kuzungumza machache na wanafunzi wanaoendelea na masomo katika shule hiyo na kuweza kuwasaidia vifaa vya michezo kama mipira huku wakipanda miti kwaajili ya kumbukumbu.
 Mwalimu Leornad Chintowa akiwakaribisha baadhi ya wanafunzi waliopata kusoma katika shule ya Sekondari ya Bwawani inayomilikiwa na jeshi la Magereza nchini mara baada ya kuwasili kwa waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo mapema leo.

Waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Magereza nchini waliweza kutoa miche 30 ya miti kwaajili ya kupandwa shule hapo huku wanafunzi wakishukuru kwa kupokea mipira kama zawadi kutoka kwa kaka na dada zao waliotangulia shuleni hapo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...