Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Gilbert Simya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Mbinga Robert Mageni waliosimama nyuma wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa chama cha albino wilaya ya Mbinga, baada ya kukabidhi msaada wa mafuta yenye thamani ya shilingi laki 8 yaliyotolewa na chama cha walemavu wilayani humo kwa ufadhili wa hospitali ya KCMC ya mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Mbinga mkoani Ruvuma Robert Mageni,akiteta jambo na mtoto mwenye ualbino ambaye hakufahamika jina lake mara moja wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa mafuta maalum ya kuzuia magonjwa kwa watu wenye ulamavu wa ngozi yaliyotolewa na chama cha albino wilaya ya Mbinga. 
Sista Judith Mwageni wa shirika la mtakatifu Wiliam jimbo la Mbinga akiwatambulisha watoto wenye ualbino wanaolelewa na kanisa katoriki jimbo la Mbinga wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa mafuta maalum ya kuzuia magonjwa ya ngozi yaliyotolewa na chama cha walemavu wilaya ya Mbinga.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Mbinga Robert Magenj akizungumza jana katika hafla ya kukabidhi mafuta maalum kwa watu wenye ualbino yaliyotolewa na chama cha walemavu wilaya ya Mbinga kwa ufadhili wa hospitali ya KCMC ya Moshi,katikati ni katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Gilbert Simya.
Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Gilbert Simya akitoa mafuta maalum ya kuzuia magonjwa kwa watu wenye ualbino jana wakati wa kukabidhi msaada wa mafuta wenye thamani ya shlingi laki 8 yaliyotolewa na chama cha walemavu wilayani humo.Picha na Muhidin Amri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...