BENKI ya NMB imeendelea kutoa elimu kwa viongozi wa Halmashauri, Manispaa,
Majiji na wananchi wa kada mbalimbali juu ya huduma za kibenki ambazo wamekuwa
wakizitoa kupitia mkutano mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala na Serikali za Mitaa (ALAT)
unaofanyika kitaifa mjini Musoma mkoani Mara ambapo wajumbe zaidi ya 500
wanahudhuria mkutano huo.
Benki hii imetoa elimu kwa viongozi wa Halmashauri, Manispaa,
Majiji na wananchi wa kada mbalimbali juu ya huduma za kibenki katika Mkutano mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala na Serikali za Mitaa (ALAT)
unaofanyika kitaifa mjini Musoma mkoani Mara ambapo wajumbe zaidi ya 500
wanahudhuria mkutano huo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, George Simbachawene akisalimiana
na meneja wa NMB tawi la Musoma, Sebastian Kayanga alipokuwa anaingia kwenye ukumbi
wa Mikutano wa Mwembeni Complex kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Mkutano wa mwaka
wa ALAT Taifa. NMB imedhamini mkutano wa ALAT Taifa kwa shilingi Milioni 206
ikiwa ni gharama za mkutano na zawadi kwa ajili ya Meya bora wa Mwaka. Pichani kulia
ni Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya ziwa, Amos Mubusi.
Kupitia mkutano huo NMB imeelezea jinsi ilivyounganisha mfumo wake wa kibenki
na mfumo wa serikali za mitaa (LGRCIS) kufanikisha ukusanyaji mapato ya kwa
wakati na bila kupotea na kuandaa vituo vya makusanyo ya fedha kusaidia
serikali katika makusano.Akitoa mada kwenye mkutano huo ulioingia siku ya 2 hii
leo,Afisa Mkaguzi Mkuu wa ndani wa (NMB) Augustino Mbogella,amesema licha ya
kusaidia serikali katika suala zima la ukusanyaji wa mapato, benki hiyo pia
imesaidia miradi ya maendeleo ya jamii ikilenga zaidi katika utoaji wa misaada
katika sekta ya elimu na afya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) George Simbachawene,akisaini
kitabu cha wageni kwenye banda la NMB kwenye maonyesho ya ALAT.
Mkaguzi Mkuu wa ndani wa
(NMB) Augustino Mbogella (pichani),amesema licha ya kusaidia serikali katika suala zima
la ukusanyaji wa mapato, benki hiyo pia imesaidia miradi ya maendeleo ya jamii
ikilenga zaidi katika utoaji wa misaada katika sekta ya elimu na afya.
Mbogella
amesema mwaka 2015 pekee zaidi ya shule 140 za msingi na sekondari zilipata
zaidi ya madawati 7,000 kwa Tanzania nzima katika mpango wa kuendelea kutatua
tatizo la madawati mpaka kufikia septemba 2016 tayari wametumia zaidi ya
milioni 900. “Upande wa afya tumetoa vifaa mbalimbali kwenye hospitali 50 za
serikali pamoja na vituo vya afya ambapo kiasi cha fedha takribani shilingi
milioni 200 zilitumika” alimalizia Augustino Mbogella.
Wakati
huo, viongozi na wananchi wameombwa kutembelea banda la NMB ili kuweza kupata
elimu zaidi likiwemo pia suala la ufunguaji wa akaunti mbambali kwenye benki
hiyo ambazo zina manufaa makubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...