Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
inatumia fursa hii kufafanua kwamba, msimamo alioutoa Msajili wa Vyama vya
Siasa Jaji Francis Mutungi (pichani) kuhusu mgogoro wa uongozi katika chama cha CUF una maana kwamba, kwa
mujibu wa taarifa zilizowasilishwa kwake na pande mbili zinazosigana na
kwa mujibu wa Katiba ya CUF toleo la 2014, Msajili alijiridhisha kwamba,
Profesa Lipumba bado ni Mwenyekiti halali wa Taifa wa chama cha CUF, kwa sababu
alitengua barua yake ya kujiuzulu kabla haijakubaliwa na mamlaka yake ya
uteuzi, kama inavyoelekeza ibara ya 117(2).
Aidha,
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inaviasa vyombo vya habari kufanya jitihada
za kuelewa msimamo wa Msajili wa Vyama vya Siasa, badala ya kuandika habari au
makala zinazopotosha umma.
Hivyo,
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inatumia fursa hii pia, kukanusha taarifa
zinazoenezwa katika vyombo vya habari ikiwamo mitandao ya kijamii kwamba, "Msajili wa Vyama vya Siasa amesema kuwa, hakumrudishia Profesa Lipumba
Uenyekiti wa Taifa wa CUF, bali Profesa Lipumba kajirudisha mwenyewe kinyemela".
Habari hiyo siyo ya kweli, imepotoshwa kwa makusudi. Watanzania wanapaswa
kuipuuza.
Ofisi
ya Msajili wa Vyama vya Siasa inawaasa viongozi wa kitaifa wa chama cha CUF,
kusoma kwa makini msimamo uliotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa na
kuuheshimu, kwani kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258, Msajili
wa Vyama vya Siasa anao wajibu wa kujiridhisha kwamba, mabadiliko yoyote
yaliyofanywa katika uongozi wa taifa wa chama cha siasa, ni halali na
yamefanywa na mamlaka halali kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za chama husika.
Sisty L.
Nyahoza
Kny: MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
26
Septemba, 2016
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...