Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa anaendelea kuisimamia timu ya wataalam na Makandarasi kurejesha mawasiliano ya barabara ya Lindi - Dar es Salaam ambapo tayari eneo la somanga limeanza kupitika na amesisitiza kuwa ifikapo kesho Alhamisi mawasiliano ya barabara hiyo yatarejea.

Bashungwa amezungumza hayo Mei 08, 2024 Mkoani Lindi wakati akisimamia zoezi la urejeshaji wa miundombinu ya barabara hiyo ambayo iliharibiwa mvua za El-Nino juzi Jumamosi zilizombatana na Kimbunga Hidaya.

“Kwa namnna tulivyojipanga tuliahidi watanzania kuwa hadi kufikia Alhamisi barabara hii tutakuwa tumerudisha mawasiliano na tayari kipande cha Somanga kilichokuwa kimekatika kwa mita 200 tumeshakikamilisha na hivi sasa nguvu zote tunazielekeza katika eneo la Songas na kuendelea katika maeneo mengine”, ameeleza Waziri Bashungwa.

Aidha, Bashungwa ameeleza changamoto zinazowakabili wataalam ambao wanaendelea kurejesha mawasiliano katika barabara hiyo ni upatikanaji wa mawe ambayo yanafuatwa Kigamboni na Boko-Magereza mkoani Dar es Salaam, huku zoezi hilo likifanyika usiku na mchana.

“Lakini kwa vile zoezi hili tunalifanya usiku na mchana pamoja na changamoto hizi tumeweza kurudisha mawasiliano eneo la Somanga na nguvu hiyohiyo tunaiamisha katika maeneo mengine”. Ameeleza Waziri Bashungwa.

Pamoja na hayo ameipongeza timu ya wataalamu ikiongozwa na Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Makandarasi na wasaidizi wake pamoja viongozi wa Wizara na Mkoa.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack amepongeza timu ya wataalam na Makandarasi kwa kufungua eneo cha Somanga ambapo amesema ana imani na eneo la Songas napo mawasiliano yataweza kurejea usiku wa leo.

Kwa upande wake Mwenyejiti wa Kijiji cha Somanga kusini, Mustafa Omari Mkunga ameishukuru Serikali kwa kazi kubwa katika eneo la Somanga ambalo lililkuwa korofi na sasa limeweza kupitika.









RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi na Viongozi mbalimbali katika Sala ya Maiti ya Marehemu Asha Simba Makwega Muasisi wa UWT pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Sala hiyo iliyoongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, iliyofanyika katika Msikiti wa Maisara Wilaya ya Mjini Unguja na kuzikwa Kijijini kwao Pete Mkoa wa Kusini Unguja leo 8-5-2024.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kutowa mkono wa pole kwa Wanafamilia ya Marehemu Asha Simba Makwega, baada ya kumalizika kwa maziko hayo yaliyofanyika katika Kijiji cha Pete Mkoa wa Kusini Unguja leo 8-5-2024.
(Picha na Ikulu)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa sekta binafsi nchini kuongeza uwekezaji na upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Rais Samia amewataka kuleta teknolojia rahisi itakayowezesha wananchi kupata nishati safi kadri ya uwezo wao pamoja na kulipia kulingana na matumizi kama inavyofanyika katika umeme.


Rais Samia ametoa wito huo leo katika hafla ya uzinduzi wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa Mwaka 2024 -2034 iliyofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).


Rais Samia pia amesema Mkakati huo unatoa mwongozo wa kitaifa kwa wadau wote kuhakikisha nchi inafikia lengo ililojiwekea la 80% ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


Vile vile, Rais Samia amesema lengo la Mkakati huo likitekelezwa na kutimia litapunguza gharama ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuongeza upatikanaji na uwekezaji wa nishati safi.


Rais Samia amebainisha kuwa Mkakati huo wa kitaifa pia utachangia jitihada za Serikali za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kutokana na uharibifu wa misitu ambao huchangiwa na shughuli za kibinadamu.


Kwa sasa, inakadiriwa kuwa takribani hekta 469,000 za misitu hupotea kila mwaka ambapo nishati za kuni na mkaa ni moja ya chanzo kikuu cha kutoweka kwa misitu hiyo.


Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri wa Maji Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Shaib Hassan Kaduara Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri wa Nchi, Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi, Wananchi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipiga makofi na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko pamoja na Waziri wa Nchi, Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo mara baada ya kuzindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024.


Wageni pamoja na Wadau mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2024.
Meneja wa Kanda ya Pwani , Vicky Mollel akipokea Mwenge wa Uhuru wakati wa mapokezi ya Mwenge Jijini Dar Es Salaam. Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Wilaya tano za Mkoa wa Dar Es Salaam kuanzia tarehe 08- 12 Mei 2024.

MAMLAKA ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imeshiriki katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru uliowasili jijini Dar es Salaam leo, Mei 8, 2024, utakaokimbizwa katika Wilaya tano za Mkoa huo.

Akizungumza kuhusu Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024, Meneja wa PPRA Kanda ya Pwani, Bi. Vicky Mollel amesema Mamlaka hiyo imepata nafasi ya kutoa elimu kupitia ujumbe unaotolewa na Itifaki ya Mwenge inayohusu matumizi ya Mfumo wa NeST.

Bi. Mollel amesema zaidi ya asilimia 90 ya miradi inayofunguliwa na Itifaki ya mwenge wa Uhuru ni miradi ya Serikali. Hivyo, utekelezaji wa miradi hiyo unatakiwa kuzingatia Sheria ya Ununuzi wa Umma na kwamba michakato ya ununuzi wake inapaswa kutumia Mfumo huo.

“Sheria ya Ununuzi wa Umma imewekwa ili kuhakikisha thamani ya fedha inapatikana katika ununuzi ndani ya Serikali. Lakini, ili kuhakikisha kuwa kuna uwazi, uwajibikaji na ushindani wa haki unaochagiza upatikanaji wa thamani ya fedha, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imejenga Mfumo wa NeST na kuagiza kila taasisi ya umma kufanya ununuzi wake ndani ya Mfumo huo pekee,” amesema Bi. Mollel.

Ameongeza kuwa, baada ya kushiriki mapokezi hayo, PPRA itatoa elimu katika Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu Mfumo wa NeST na Sheria ya Ununuzi wa Umma. Alifafanua kuwa elimu hiyo itatolewa katika maeneo mbalimbali ambayo wananchi watakusanyika kwa ajili ya Mbio za Mwenge ambapo Mamlaka hiyo itaweka banda maalum la kutoa huduma.

Mwenge wa Uhuru unakimbizwa katika mkoa wa Dar es Salaam kwa siku tano katika Wilaya za Ilala, Temeke, Kigamboni, Kinondoni na Ubungo.

Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Profesa Ibrahim Lipumba akizungumza leo Mei 08, 2024, wakati wa kufungua Mkutano wa Kitaifa wa Kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu y Sheria za Uchaguzi zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Bernadetha Kafuko akizungumza leo Mei 08, 2024, wakati wa kutambulisha uwepo wa Kitaifa wa Kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu y Sheria za Uchaguzi zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. 
Balozi wa Marekani, Bw. Michael Battle akizungumza kwenye Mkutano
wa Kitaifa kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu ya sheria za Uchaguzi
zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025. katika Ukumbi wa Maktaba mpya, Chuo kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM).
Balozi wa Uswis Nchini, Didier Chassot, akizungumza kwenye Mkutano
wa Kitaifa kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu ya sheria za Uchaguzi
zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.katika Ukumbi wa Maktaba mpya, Chuo kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM).
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe akizungumza kwenye Mkutano wa Kitaifa kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu ya sheria za Uchaguzi zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.katika Ukumbi wa Maktaba mpya, Chuo kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM).
Baadhi ya Wadau wa Demokrasia wakiwa katika ufunguzi Mkutano wa Kitaifa wa Kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu y Sheria za Uchaguzi zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. 



Picha za pamoja.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
KUELEKEA uchaguzi wa Serikali za Mtaa Oktoba, 2024 hofu ya tanda juu ya nani atasimamia Uchaguzi wa huo kati ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) au Tume huru ya Uchaguzi ambayo imeteuliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza wakati wa kufungua Mkutano wa Kitaifa wa Kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja juu y Sheria za Uchaguzi zilizopitishwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuwa hakuna dalili zozote zinazoonesha tume huru ya Uchaguzi inajiandaa kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.

Amesema hotuba ya bajeti ya Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) imeeleza kuwa inaratibu Maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye vijiji 12318, mitaa 4263 na Vitongoji 64361 katika halmashauri 184 utakapfanyika 2024.

Wameshatekeleza shughuli za maandalizi ikiwa pamoja na uhakiki wa maeneo ya Utawala yatakayoshiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu wa 2024.

Hivyo wameshaandaa rasimu ya tangazo la Serikali kuhusu maeneo hayo ya utawala na kuandaa rasimu ya kanuni za uchaguzi na kufanya mipango yandani ya Serikali kupata maoni ya yakujumlisha katika rasimu hiyo.

Lakini mpaka sasa Vyama vya Siasa havijashirikishwa katika maandalizi ya kanuni ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Waziri alieleza katika mwaka 2024/2025 ofisi ya Rais TAMISEMI imetenga shilingi milioni 17.8 kwaajili ya kuratibu na kusimamia Uchaguzi wa serikali za Mitaa wa 2024.

Kwahiyo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utasimamiwa na TAMISEMI lakini sheria ambayo tayari imeshapitishwa inasema Jukumu la Tume Huru ya Uchaguzi ni kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Sasa Hili likoje kwamba Sheria teyari imepitishwa lakini Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utasimamiwa na TAMISEMI.

Labda wanamaelezo yanamna gani kipindi hiki cha Mpito ya TAMISEMI itashirikiana na Tume Huru ya Uchaguzi.

Awali Prof. Lipumba alisema Serikali na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limekubali pendekezo la muda mrefu la wadau wa demokrasia kuwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na tume huru ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI.

Licha ya hayo Prof. Lipumba aliwaomba washiriki na wadau wa demokrasia kuyajadili mambo hayo kwa kina ili kuweza kutoa mapendekezo yao.

"Nawaomba washiriki wa mkutano huu kujadiliana kwa uwazi kwa kutumia nguvu za hoja lakini pia kwa kuheshimiana kwa lengo la kujenga Taifa moja lenye mfumo imara wa kidemokrasia unaoendana na maadili ya watanzania.

Pamoja na kukosoana lakini pia hali ya kidemokrasia katika awamu ya tano ilikuwa na changamoto nzito, lakini falsafa ya 4R imetupa nguvu Mpya ya kujadili namna ya kujenga demokrasia ndani ya nchi yetu, ni mhimu tusiishie kwenye kuzungumza tuu, twende pia kwenye vitendo vya utekelezaji, Mkutano huu utafikia maazimio muafaka ambayo tutayawasilosha selikalini ili yaweze kufanyiwa kazi." Ameeleza

Kwa Upande wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar, Dkt. Mohamed Seif amekubaliana kuwa bunge lomeshapitisha sheria ya uchaguzi lakini amesema watafanya mapitio ili kuona kama kunamapungufu ili waweze kuyaweka sawa.

Amesema kuwa Mchakato ulivyokwenda wa kupitisha sheria ya chaguzi wa Serikali za Mtaa ulikwenda vizuri na walishiriki pamoja na vyama vyote vya siasa nchini lakini kama yatakuwepo mageuzi yoyote basi tutafanya mageuzi yatakayojitokeza na kuweka sheria sawa ili nchi iweze kwenda sawa.

"Tunataka nchi hii tuijenge kwa demokrasia na sisi bado tunaendeleza zile 4R za Mwenyekiti wa CCM taifa ili kuona nchi yetu inaishi kwa amani, usalama na Utulivu."

Kwa Upande wa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe amesema kuwa haijafanyika tathmini ya kisayansi ya kujua athari za Uchaguzi wa 2019 wa serikali za Mitaa kwa kuangalia zimeathiri vipi maendeleo ya wananchi katika kijiji, Kitongoji.

Amesema kuwa hata kama kukifanyika maboresho ya sheria kiasi gani kama upande wapili hakuna utashi wa Kisiasa, Utashi wa kisheria haya mabadiliko ya kisheria yatakuwa yanapoteza muda.

Amesema kuwa mambo yaliyofanyika katika chaguzi za Serikali za Mitaa za kuanzia 20000 hadi leo 2024 Chama Chake kimekataa kufanya kutokana na kuona mambo ya zamani yanafanyika mpaka leo.


Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akiweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.


Na.Alex Sonna-KAKONKO

JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limeishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha nyingi za maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu na majengo ili kuchukua vijana wengi wanaohudhuria mafunzo ya lazima kwa mujibu wa sheria pamoja na kundi la kujitolea

JKT ilikuwa na uwezo wa kuchukua vijana 5000 lakini kwa sasa inaweza kuchukua vijana 50,000 katika kundi hilo kwa wakati mmoja kutokana na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia kutoa fedha.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena, wakati akiweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.

Brigedia Jenerali Mabena amesema Serikali imekuwa ikiendelea kufanya hivyo toka kurejeshwa kwa mafunzo ya kundi la kujitolea.

"Ikumbukwe wakati mafunzo yale ya lazima yanarejeshwa JKT ilikuwa na uwezo wa kuchukua vijana 5000 tu lakini kwa sasa inaweza kuchukua vijana 50,000 katika kundi hilo kwa wakati mmoja,"amesema Brigedia Jenerali Mabena.

Amesema yote hayo yanatokana na JKT kuendelea kupewa fedha za maendeleo na Serikali.

Kuhusu kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Brigedia Jenerali Mabena,amesema wakati kikosi kinaanza kilikuwa hakina uwezo wa kuchukua vijana 1000 lakini kwa sasa kina chukua 4000 mpaka 5000.

"Na mimi niseme tu katika kikosi hichi tulichopo cha 824 Kanembwa Kakonko Mkoa wa Kigoma.Kikosi hichi tulikabidhiwa kutoka katika Kambi ya wakimbizi waliokuwa wanakaa hapa ilianza kuwa kiteule na baadae ikapewa hadhi ya kuwa kikosi,"amesema Brigedia Jenerali Mabena.

Amesema kikosi hicho wameendelea kukiongezea uwezo kwa kuweka mahanga ya kulala vijana pamoja na bwalo na miundombinu mingine ambayo itatumika katika kulea vijana.

Brigedia Jenerali Mabena amesema katika mwaka wa fedha ambao utaishia Juni 30,2024 kikosi hicho kimepewa Sh bilioni 1.47 ambapo fedha hizo zinatumika kwa ajili ya kuhakikisha majengo yanakuwa sawa sawa.

Amesema katika fedha hizo kikosi kinaenda kutengeneza mahanga saba yenye uwezo wa kuchukua vijana 100 kila hanga moja.

"Kwa hiyo unaona tayari kutakuwa na ongezeko la vijana 700 katika ile idadi ya 4000 mpaka 5000,"amesema Brigedia Jenerali Mabena.

Amesema kuna kituo cha Kiteule ambacho kipo Misenyi Mkoani Kagera kwa ajili ya shughuli za ufugaji

Amesema kule wana Kilimo,ufungaji pamoja na Uvuvi ambapo kitatumika kama sehemu ya kufugia na vijana watakitumia kupata mafunzo.

"Unaona kwa jinsi ambavyo Serikali imeendelea kutoa fedha na miundombinu inaendelea kukaa sawa na kuchukua vijana wote kwa wakati mmoja,"amesema

Kwa upande wake Mkurugenzi wa fedha JKT,Luteni Kanali Eveline Kibisa amesema kama Mjumbe wa kamati ya fedha za maendeleo wanawapongeza wakuu wa vikosi sehemu zote walizopita kwani majengo yamejengwa vizuri na yanathamani.

Ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa namna ambayo imewezesha kwani wameweza kuwapatia fedha za kutosha ambapo katika kila kikosi wameweza kuongeza idadi ya vijana.

"Nitoe rai kwa wakuu wa vikosi kuendelea kuzisimamia vizuri fedha hizo ili angalau Serikali ikiona kuna matumizi mazuri ipate moyo wa kuendelea kusapoti."amesema Luteni Kanali Kibisa

Nay,Kamanda wa Kikosi cha 824 KJ, Luteni Kanali Mantage Nkombe,amesema katika kikosi hicho wamepata fedha kwa ajili ya ujenzi wa mahanga saba.

"Tumeona ni mafanikio kwa sababu tunaenda kuongeza wigo na namba ya Vijana kujiunga JKT Kanembwa inaenda kuongezeka zaidi ya awali,"amesema Luteni Kanali Nkombe

Amesema kupitia fedha za maendeleo wanaenda kutekeleza miradi hiyo kwa kutekeleza maagizo kutoka Makao Makuu

"Kwa kuhakikisha majengo yanakamilika kwa wakati kulingana na fedha iliyotumwa na kuhakikisha thamani ya fedha inazingatiwa na majengo yanajengwa katika ubora na kwa muda sahihi,"amesema

Amesema wanataraji ifikapo 30 June 2024 majengo yatakuwa yamekamilika kwa ajili ya vijana wapya ambao watakuja kujiunga na JKT katika kikosi hicho.

Kuhusu faida watakayopata katika miradi hiyo,amesema:"Kimsingi ni faida na kijana anapata ujuzi na ujuzi hauzeeki na ni manufaa kwake na atatumia kujiongezea kipato".

Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akipokea taarifa ya ujenzi kabla ya kuweka wakati akiweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.

Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akiweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.



Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,(kulia) akipiga makofi mara baada ya kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.Kushoto ni Kamanda wa Kikosi cha 824 KJ, Luteni Kanali Mantage Nkombe.



Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akikagua maendeleo ya ujenzi mara baada ya kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.



Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.


Mkurugenzi wa fedha JKT,Luteni Kanali Eveline Kibisa,akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.




,akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la Msingi ujenzi wa Mahanga ya Vijana katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa,Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.

 Na. Peter Haule, WF, Dodoma

Serikali imesema kuwa ulipaji wa madai yanayotokana na kupokelewa kwa bidhaa au huduma huzingatia masharti ya mikataba ya zabuni au kandarasi iliyoingiwa kati ya Serikali na mtoa huduma.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Temeke Mhe. Dorothy George Kilave, aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali wa kuwasaidia wafanyabiashara kulipwa madai na riba wanapo cheleweshewa malipo.

 

Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali hulipa au hulipwa riba iwapo masharti ya mikataba ya zabuni au kandarasi imekiukwa.

 

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge huyo la kuitaka Serikali kutoa maelekezo ili wazabuni walipwe madai yao pamoja na riba wakicheleweshewa fedha baada ya kuingia mikataba, Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali inaangalia namna ya kuliweka jambo hilo kwenye kanuni za ununuzi ili kuwalinda wazabuni wa ndani ambao si tu kwamba wanacheleweshewa malipo yao, bali pia Wakandarasi kutoka nje wanaoingia nao mikataba ya kazi huwalipa kwa shilingi ya Tanzania wakati wao wanalipwa kwa dola za Marekani.

 

Aidha, Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali inakamilisha kanunui za ununuzi baada ya Bunge kurekebisha Sheria ya ununuzi wa umma, lengo ni kuhakikisha wakandarasi wa ndani wananufaika na kazi wanazozifanya.

 

Katika hatua nyingine, akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Mhe. Cosato David Chumi, kuhusu muda ambao Serikali itaanza kurejesha asilimia 20 (Retention) ya Kodi ya Ardhi kwenye Halmashauri kama ilivyopitishwa katika Sheria ya Fedha 2023/2024, Dkt. Nchemba alisema kuwa urejeshwaji wa kodi hiyo utaanza baada ya zoezi la kukusanya kodi ya ardhi litakapoanza kutekelezwa rasmi na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

 

“Utaratibu wa kurejesha asilimia 20 ya kodi ya ardhi kwenye Halmashauri unatarajiwa kuanza kabla au ifikapo Juni 30, 2024”, alisema Dkt. Nchemba.

 

Alisema kuwa hadi Aprili 2024, taratibu za kuwezesha halmashauri kuanza kukusanya kodi ya ardhi hazikukamilika hususan kufungamanisha mfumo wa utunzaji wa kumbukumbu za ardhi na mfumo wa kukusanya mapato ya halmashauri – TAUSI.

 

Alisema mwaka 2023/24, Serikali ilifanya maboresho ya ukusanyaji wa kodi ya ardhi ambapo halmashauri kupitia Ofisi ya Rais -TAMISEMI zinatakiwa kukusanya kodi ya Ardhi kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

 


Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akijibu swali la Mbunge wa Temeke, Mhe. Dorothy George Kilave na Mbunge wa Mafinga Mjini, Mhe. Cosato David Chumi, kuhusu mpango wa Serikali wa kuwasaidia wafanyabiashara kulipwa madai yao pamoja na riba wanapo cheleweshewa malipo na pia Serikali itaanza lini kurejesha asilimia 20 (Retention) ya Kodi ya Ardhi kwenye Halmashauri.  

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

Na Jane Edward, Arusha

Vilio, nyuso za Huzuni, Majonzi na sura zilizokufa Matumaini ni mambo yaliyotawala kwenye Nyuso za mamia ya Wakazi wa Mkoa wa Arusha waliojitokeza kwa wingi kwenye Kliniki Maalum ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda ya kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za Wananchi.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amekuwa hapa kwenye viwanja vya Ofisi yake Mkoani Arusha kuhakikisha kuwa Mawakili, watumishi wa idara mbalimbali na taasisi zinazotoa misaada ya kisheria zinawajibika kikamilifu kuwasikiliza na kutatua changamoto zote za Wananchi waliojitokeza hapa.

Makonda ameahidi kusimamia kuhakikisha kila mmoja anaridhika na maamuzi yatakayotolewa leo akiahidi pia kutoa msaada wa mawakili kwa kesi zitakazokuwa na uhitaji wa kupelekwa mahakamani.

"Leo nataka niwaambie wananchi wa Arusha hizi siku tatu ni za kwao na ninataka kila mwenye kero aje hapa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wasikilizwe na wataalamu wangu hapa kwaajili ya utatuzi"Alisema

Haya hivyo zoezi hilo limeanza leo Mei 08,2024 na likitarajiwa kukamilika Mei 10, 2024.



 

 


Top News