Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band maarufu kama
FFU ughaibuni ukipenda waite viumbe wa ajabu Anunnaki Alien juzi wikiendi walifanikiwa kuwadatisha washabiki wa muziki nchini Latvia katika maonyesho ya Summer Festival,yaliyofanyika Liga. 
Bendi hiyo yenye makao yake nchini Ujerumani inayoongozwa na mwanamuziki mahiri Ebrahim Makunja aka  Kamanda Ras Makunja,imejizolea umaarufu wa kimataifa kwa kutumia mdundo wake wa "Bongo Dansi" uliochanganywa na rumba la kukata na shoka mdundo huo umefanikiwa kuwazoa na kuwadatisha akili washabiki wengi wa kimataifa.
Ngoma Africa Band kwa sasa wanatamba na single CD yao mpya 'La Mgambo"
yenye mbili za kumuaga Rais JK.
Unaweza kuwasikiliza at www.reverbnation.com/ngomaafricaband au uungana nao at www.facebook.com/ngomaafricaband
 Gwaride limenoga Latvia katika maonyesho ya Summer Festival,yaliyofanyika Liga. 
 Mashabiki wa Latvia katika maonyesho ya Summer Festival,yaliyofanyika Liga. 
 Mambo ya Latvia katika maonyesho ya Summer Festival,yaliyofanyika Liga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ngoma Afrika band aka ffu-ughaibuni aka watoto wa mbwa viumbe wa ajabu Anunnaki naona maafande wakisukuma gwaride mbele kwa mbele

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...