Na Bashir Yakub
Sheria  ya  Uwekezaji  ya  Mwaka  1977 imehamasisha  uwekezaji  kwa  wazawa  na  wasio  wazawa  kwa  kuweka  mazingira  rafiki  kwa  wajasiriamali katika  nyanja  zote.  Wapo  ambao  wanajua fursa hizi  na wamezitumia   kujipatia  maendeleo  na  wapo  ambao  hawajatumia  fursa  hizi.  Nataka  niseme  kitu  kimoja  kuwa  wazawa  wengi  wameshindwa  kufanikiwa  kwa  kutojua  uwepo wa fursa. Wengi  wangependa  kutumia  fursa   kama  zipo  lakini  hawajui ziko  wapi na  zinapatikana vipi.
Badala  yake  wageni  na  watu  wengine  ambao  si  wenye  asili  halisi  ya  Tanzania  ndio  wamekuwa  wakihabarishana  kuhusu  fursa  hizi  wanazitumia  na  wanafanikiwa sana.  Wenyeji  halisi   wa  nchi  hii  wanabaki  kutazama  mafanikio  ya  watu  hawa  wasijue  yanapatikanaje. 
Ziko  fursa  ambazo  zimetolewa  na  serikali  na  kuainishwa  na  sheria  mbalimbali  mojawapo  ikiwa  hii  ya  kusamehewa  kodi  kwa bidhaa  zinazoingizwa  nchini  kutoka  nje  ya  nchi. 
Wafanyabiashara  watakubaliana  na  mimi  kuwa  ikiwa  utapata  msamaha mzuri  wa  kodi bandarini  basi  unayo  nafasi  kubwa  ya  kutengeneza  faida  kubwa  katika  biashara  yoyote  utakayoamua  kufanya.

Mara  zote  kodi  ndio  huwa  tatizo. Makala  haya yataeleza  namna  ya  kupata  msamaha  wa  kodi. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...